Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na wimbi kubwa la mafundisho potofu nchini Tanzania. Kama inavyoonywa katika Mathayo 24:24 na 12:39, jamii nyingi zimejikita katika kutafuta ishara na miujiza badala ya msingi sahihi wa kiroho. Hii imesababisha watu wengi kupotezwa na manabii wa uongo, na hatimaye kupoteza mwelekeo wa maisha yao.
Kila mtu ana hiari ya kuamini anachotaka, lakini lengo letu ni kukusaidia kufanya maamuzi sahihi. Tunajitahidi kukufundisha jinsi ya kutofautisha kweli na uongo kwa kusimama kwenye msingi wa Neno la Mungu. Ahadi yetu katika Kristo ni moja: kukufundisha kweli yote itakayokuletea uhuru wa kweli katika maisha yako ya kila siku.